Ufahamu Ugonjwa wa miguu kuwaka moto
Ufahamu zaidi ugonjwa wa miguu kuwaka moto Katika mwili wa binadamu, kuna tatizo la kiafya ambalo huambatana na dalili za mtu kuhisi maumivu, kuhisi kuwaka moto na kufa ganzi kwa viungo vya pembezoni mwa mwili yaani miguu na mikono. Tatizo hili kitaalamu hujulikana kwa jina la Peripheral Neuropathy. Matatizo haya ya kiafya (miguu/mikono kuhisi ganzi, baridi au maumivu) husababishwa na kuumia au kudhoofika kwa neva za pembezoni mwa mwili (miguuni au mikononi) na hivyo kupotea kwa uwezo wa kufanya kazi wa neva katika sehemu husika, miguuni au mikononi. **Dalili zinazoambatana na ugonjwa huu ni hizi zifuatazo* 1.Mtu kuhisi ganzi 2. kushindwa kushika au kunyanyua kitu, kuchoka kwa misuli na kadhalika. 3.maumivu au kuwaka moto maeneo ya miguuni/mikononi, Miongoni mwa mambo ambayo hupelekea neva hizi za pembezoni kudhoofika na kushindwa kufanya kazi vizuri ni haya yafuatayo: 1.Kupungua kwa virutubisho mwilini,hasa mkusanyiko wa vitamini B, (Vitamin B Complex). 2.Matumizi ya dawa, mfano daw
Maoni
Chapisha Maoni